Thursday, February 21, 2008

Rush Limbaugh Went Hard on African Aide

CALLER: No, no, no, you don't hear me Rush, you don't hear me say anything when it comes to Africa. You don't hear me say anything against George Bush. He do well. He come to Senegal where I'm originally from two years ago. I respect what he do for Africa, but I'm saying, I'm saying all these years, I'm not talking about the George Bush years, I'm talking about since I was a kid, you heard commercials, everything saying lets help Africa, nothing get done, because what happened is you don't put the help in the right hands. You always put it in the government who are in charge over there and (unintelligible)

RUSH: Amen, bro. Amen. I agree with you a hundred percent. In fact, I think the best thing could happen for Africa is to have the aid cut off for like five years because two things have happened, and you're right. The money that has been given in previous years by this country and UNICEF and all the other worldwide organizations, all the money, all the time, all the caring, all the compassion to save Africa, and it's still this place that's miserable, we are told, it's going to hell in a handbasket, "Why don't we do something for Africa?" Rock stars are resurrecting their careers on saving Africa. And yet, it's sort of like the poor in this country, we've thrown everything, we've given them the kitchen sink after throwing it at them, and still have the poor and we still have the disadvantaged. At some point, you gotta get the money into the hands of the people who are going to use it for investment and growth, not welfare, and you have to take it out of the hands of these despot warlord thug dictators in these countries that are getting their hands on it, people like Mugabe in the former Rhodesia, now Zimbabwe. Africa has become a worldwide welfare state with the welfare recipients primarily made up of the thug dictators running some of these countries and oppressing their people. There is no reason in the world today why the vast majority of the Third World is in one continent. There's no reason for it whatsoever. But I'll tell you who you can blame, Al Haji, guess who's preventing development there? Our good old American environmentalists, our leftists who prefer squalor to advancement, to running water, to electricity, "because that requires fossil fuels, Mr. Limbaugh, and that's destroying the planet." So people in Africa have to live in pigsties because they're not allowed to develop the country by Americans and liberals all over the world who are standing in their way. George Bush has gone over there, and he has said, "We got new rules. We're going to continue to give you the aid. You gotta show us something for it," and he's being celebrated upon his arrival. The Drive-By Media here cannot understand it. But the people of Africa do. They understand what's happened with his presidency in that regard. But the idea here that Barack Obama is the magic elixir that you can assign to any problem and it automatically gets fixed -- you know, the thing that worries me in a situation like that when you have people of a cult, nothing ever does have to get fixed. It's sort of like liberals and their good intentions. That's all that matters. All you have to do is, "I want that problem solved, Mr. Limbaugh! I can't bear to see people --" Okay. Well, good, we'll spend some money on that. Good. And they think the problem is solved. Their good intentions got it done. So you can throw under the canvas, the black canvas that is Barack Obama any problem, and you make him the solution to it, and whether it gets solved or not, you think he's great because you've made him into what he is, not him. That's the appeal here. Look, Al Haji, nice to have you on the program. I'm glad you called

full story at: http://www.rushlimbaugh.com/home/daily/site_022008/content/01125110.guest.html

Wednesday, February 20, 2008

Jamboforums Chombo Cha Ugaidi Adai IGP Mwema

katika press conference jana IGP mwema alifafanua kisa cha kuwashikilia wana Jamboforum wawili. Akielezea kwa mbwembwe kabisa kwama jamboforum ni chombo cha kigaidi, mkuu huyo wa polisi alionyesha dhahiri kabisa kutofahamu kwakwe maana ya neno forums.

Hata hivyo mkuu huyo hakuzungumzia ni kwa nini hajamsweka lupongo Rostam Aziz, Jitu Patel au David Balali mpaka dakika hii. Hili limeonyesha ni jinsi gani kisiwa cha amani Tanzania kinavyotawaliwa na wababe wachache. Vilevile IGP huyo hakuelezea ni nini hitimisho la kampuni hewa za Kagoda, au Richmond.

Baadhi ya watanzania wengi waliojiwa na blog hiii walishangazwa kuona ya kwamba ni kwanini wezi wa shillingi million 152 kwa siku hawapo kizuizini mpaka leo. Na wanaokamatwa ni wale walio lia kwa miaka miwili mfululizo kuhusu wizi wa Richmond. Jee muheshimiwa IGP hii ndio haki sawa kwa wote? Jee aliyechafuliwa jina ni Rostam Azizi au Jitu Patel au? Na kama ni hao jee ni kwa nini usiwataje hadharani? Jee muheshimiwa IGP unamausiano gani na watu hao walio dai wamechafuliwa majina yao mpaka usiwataje?

Ni ufahamu wangu mdogo ya kwamba huitaji degree ya sheria ya Havard kufahamu ya kuwa muheshimiwa IGP na wenzie wametumia madaraka waliyonayo kusurpress democrasia. Wametumia jeshi na vifaa vyao vya moto kunyanyasa watanzania wachache. Jee kwa mwendo huu tutafika? Kama mtoa maoni anakwenda jela wakati Ditopile anatamba na STJ mtaani jee hiyo ni haki?

Ni wito wa wana Jamboforum kuzungumzia swala hili katika arena ya kimataifa, ni muda muwafaka kuwaumbua mandumilakuwili hawa, mandumilakuwili wajifanyao wao ni wapenda demokrasia kumbe ni madikteta. Ni muda muafaka wa kuwavua vilemba vyao vya ukoka vya kujidai wanaipenda Tanzania, kumbe wanapenda madaraka yao. Haki sawa kwa wote? Hii ni kauli ya muheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, Jee haki ipo wapi? Jee ni haki hagi ambayo wengine wamekula zaidi ya million 500 na wapo mitaani, na wengine wameuwa raia kwa kusudia na wapo mtaani, na wengine wamechangia maoni yao kwenye mtandao na wako jela?

Kwa mwendo huu tunatofauti gani na iddi Amini Dada aliyewapa wahindi masaa kadhaa watimuke Uganda? Swala la kuifunga Jamboforum halina tofauti na swala la kumwagia waandishi tindikali. IGP tunaomba ufuatilie maswala yanayo ikwanza nchi kuendelea, na sio maswala yanayotia chachu maendeleo ya nchi.
Tunaomba Mh. Mwema ukamate wezi walioibia walipa kodi mabillioni ya shillingi na sio wachangiaji wa mtandao. Swala hili ni sawa na ukiukaji wa haki za msingi za binadamu, ni sawa na kuendesha gereza la siri la kutesa watu.

Jamboforums.blogspot.com copywright 2008

Mh Pinda Akabidhiwa Office


Waziri Mkuu wa zamani Mh. Lowassa jana alikabidhi office ya waziri mkuu rasmi.
Akipeana mikono kwa utashi mkuu na waziri mpya Mh. Mizengo Pinda, bunge huyo wa Monduli alionekana kuwa mwenye furaha na tabasamu usoni.

Jeshi La Polisi Lacheza Kizungu Mkuti.

Ikiwa ni masaa kadhaa tangu wana Jamboforums kuachiwa kwa dhamana na jeshi la polisi. Ni kweli ya kwamba jeshi hilo liliwashikilia Watanzania hawa kwa misingi ya kibabe, misingi ya kijesusi ambayo imetumika zama zile za ulanguzi na ubepari. Akihojiwa na BBC swahili (www.bbc.co.uk/swahili) mzungumzaji mkuu wa jeshi hilo alionekana kujitafuna tafuna pasipo kueleza ni nini makosa ya wana Jamboforums hao.

Habari tulizonazo kutoka klh news (www.klhnews.com) zinathibitishwa kuachiwa kwa wana jamboforums hao. Vile vile wana jamboforum wengi duniani wamenukululiwa kukikemea kitendo hicho cha kikoloni cha kukamata watu pasipo hatia. Hata hivyo jeshi la polisi limeendelea kutupakazia wana jamboforum mambo yasio na kichwa wala miguu, mambo kama Jamboforum ni website ya ngono, ni website ya kigaidi na mengine mengi.

Wito wa wana Jamboforum kwenda kwa wanaserikali ni kwamba, Jamboforum haina mahusiano yoyote na chama chochote cha kisiasa nchini Tanzania, Jamboforum haitokufa wala haitodhibiti haki ya wanchi kuzungumza, jamboforum haitoacha kukemea, kukosoa na kushutumu vitendo vyovyote vile vya kinyonyaji vitakavyofanywa na serikali ya awamu yoyote au ya chama chochote nchini Tanzania. Vile vile jamboforum itaendeleza wimbi lake lile lile la kusifia maamuzi mazuri ya serikali pindi yafanyikapo, na vile vile kukosoa maamuzi ya kihayawani kama Richmond, IPTL, Dowas, na Mengine mengi.

Kila mwanadamu ana haki ya kuzungumza iwe ni kwa ana kwa ana, au iwe kwa kutumia nick name kwenye internet au iwe kwa kutumia jina lake kwenye gazeti, si haki ya serikali huru yoyote kuzuia uhuru wa kusungumza. Imefika muda kukemea mambo haya ya kijasusi ambayo jeshi la polisi la Tanzania linayafanya. Kukamata vijana hawa kuna tofauti gani na kumwagia waandishi tindikali? karne ya ishirini na mmoja inahitaji serikali yenye ufanisi wa mambo yake, na sio serikali yenye miundo mbinu ya kijasusi.

Mungu ibariki Africa, Mungu ibariki Tanzania.
Asanteni

Tuesday, February 19, 2008

Tanzania Yarudi Enzi za Communism, Yakamata Wana JamboForum kwa Kigezo Cha Usalama

Katika karne hii ya ishirini na moja, karne ambayo sayansi na techenolojia ndio chombo pekee mbadala. Karne ambayo internet inawasogeza walio mbali kuwa karibu, internet inawavutia wasio na sauti kuwa na sauti, karne ambayo internet inawapa habari wasio na habari.
Hali ni tofauti nchini Tanzania, baadhi ya Wanatanzania wenzetu walishikiliwa na usalama wa Taifa kwa kisa cha kutumia haki yao ya kuongea pasipo kuvunja sheria.

Serekeli ya Mh. Jakaya Kikwete imetumia udictator kukamata raia wasio na hatia kwa kisingizio cha usalama. Mambo haya ya kinazi tumeyaona kwenye enzi za Hitler, na enzi za umoja wa nchi za Urusi katika karne hizo. Ni wazi kwamba CCM wanashindana na watu wasio wafahamu, ni sawa na kupigana na upepo. Kukamata wachangiaji katika internet sio dawa ya kuzuia watu kuzungumza mawazo yao, bali ni chachu ya kuwaamsha watanzania wengi kuingia kwenye mchakato huu.

Ni imani yangu kwamba serikali ya Mh. Jakaya Kikwete itawapa immunity hawa Watanzania wenzetu, na kukomesha mchezo huu wa kinazi kwa Watanzania wengine. Ni fika ya kwamba katika dunia ya leo Tanzania haiwezi kuafford adhabu za kuzuia haki ya uhuru wa kuzungumza.

Tanzania haiundwi na kundi la watu kumi au elfu moja, Tanzania inaundwa na watanzania zaidi ya million 36, hivyo kila mtanzania ana haki ya kuzungumza lile adhanialo ni muhimu kwa maoni yake pasipo kuvunja sheria. Watanzania hawa hawajavunja sheria, hivyo basi tunaomba waachiwe mara mmoja na wafutiwe mashitaka dubya yaliyoanzishwa.

Ni wazi kwamba Mh. Jakaya Kikwete amesifika katika Dunia kwa kuipa media haki ya uhuru, japokuwa swala hili limetia doa kwa serikali ya Mh. Jakaya Kikwete. Vilevile ni ufahamu wangu kwamba serikali ya Tanzania inafahamu nguvu ya internet, hivyo basi mimi kama Mtanzania natoa wito mmoja tuu, nao ni "Hao waliofunguliwa mashitaka wafutiwe mara moja" kabla hatujaomba msaada wa Internationa Media kama Associate Press kutusaidia kupressurize swala hili katika International Arena.

Lengo sio kuigawa Tanzania, Lengo ni kuunda Tanzania ya umoja na Amani. Tanzania inayoheshimu haki kwa wote, Tanzania inayofuata kanuni na misingi za uhuru wa wananchi. Karne hii ya ishirini na mmoja tunaitaji kwenda mbele na sio kurudi enzi za communism.